Michezo
Manchester United yaingia hatua ya robo fainali ya michuano ya FA
Klabu ya Manchester united jana imefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali ya michuano ya FA baada ya kupata ushindi dhidi ya Shrewsbury Town wa mabao 3-0.
Manchester united magoli yalifungwa kupitia wachezaji wake Chris Smalling, Juan Mata na Jesse Lingard.
Baada ya ushindi huo sasa Manchester united itakutana na West Ham United katika hatua ya robo fainali Mechi ambazo zinatarajia kuchezwa wikiendi ya Machi 11 na 14 mwaka huu.
Huku Chelsea itakutana na Everton katika mchezo wa Robo Fainali baada ya kuiondoa Manchester City, Crystal Palace wakiongozwa na wao watasafiri kuikabili Reading, Watford watakuwa wageni kati ya Arsenal au Hul