Michezo

Manchester United yammendea kiungo wa Real Madrid, Di Maria kwa dau la £25m

Klabu ya Manchester United ipo tayari kutoa kiasi cha £25million kwaajili ya kumsajili Angel Di Maria baada ya winga huyo kukiri anaweza kuiacha Real Madrid.

Real Madrid - Training Session And Press Conference

Kwa mujibu wa mtandao wa Merto Sport, maafisa wa Old Trafford wamemuweka Di Maria kuwa miongoni mwa wachezaji wa juu kwenye orodha ya majina ya wachezaji ambayo wanayafanyia kazi. Pia kwa mujibu wa ripoti za Hispania, United wapo tayari kutoa £25million na zaidi ili Di Maria aweze kutua Old Trafford.

Di Maria, ambaye alifunga mabao 11 na kuisaidia Real Madrid msimu uliopita amesema ana furaha kuendelea kuichezea Real Madri na pia anaweza kuiacha klabu hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents