Michezo
Manchester United yamsajili mlinda mlango wa Argentina, Sergio Romero
Manchester United imefanikiwa kumsajili kipa namba moja katika timu ya taifa ya Argentina, Sergio Romero mwenye umri wa miaka 28. Mlinda mlango huyo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia Manchester United.
Romero ambaye ni mchezaji huru ametua Man United kuchukua nafasi ya Victor Valdes atakayeondoka majira haya ya kiangazi.
Romero alikuwa sehemu ya kikosi cha AZ Alkmaar kilichobeba ubingwa wa ligi ya Uholanzi mwaka 2009 chini ya Louis van Gaal.