Michezo
Manchester United yamsajili Victor Valdes
Kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdes amekubali kujiunga na klabu ya Manchester United.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Spain, ambaye amekuwa akifanya mazoezi na Manchester United kwa zaidi ya miezi miwili katika jitihada za kupona jeraha la goti, amekubali mkataba wa miezi 18.
Valdes, 32, alishinda makombe sita ya La Liga, na matatu ya Champions League akiwa na Barcelona, kabla ya mwisho wa msimu uliopita ambapo mkataba wake ulimalizika.
Mkataba huu huenda ukasababisha kipa wa akiba wa United Anders Lindegaard kuondoka Old Trafford.
With thanks! Valuable information!
With thanks! Valuable information!