Michezo
Manchester United yathibitisha kuwasajili Morgan Schneiderlin na Bastian Schweinsteiger
Klabu ya Manchester United imefanikiwa kukamilisha usajili wa wachezazaji wawili. Wa kwanza ni Morgan Schneiderlin mwenye umri wa miaka 25 kutoka Southampton. Kiungo huyo Mfaransa anahamia Old Trafford kwa dau la pound milioni 25 kwa mkataba wa miaka minne.
Morgan Schneiderlin
Mashetani hao wekundu wamethibitisha pia kumsajili Bastian Schweinsteiger kutokea klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani. Manchester United wamekwea pipa kuelekea Marekani katika ziara ya maandalizi ya msimu mpya ‘Pre-season’ wakiwa na wachezaji wao wapya.
Bastian Schweinsteiger
Wachezaji wa Manchester United wakiwa ndani ya ndege kuelekea Marekani