Michezo
Manchester United yatinga nusu fainali FA
Klabu ya Manchester United itacheza na Everton katika nusu fainali ya Kombe la FA kwenye Uwanja wa Wembley baada ya kuifunga West Ham United.
Marcus Rashford alifunga goli la kuongoza katika robo fainali hiyo dakika ya 54 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Anthony Martial naye Marouane Fellaini alifunga goli la pili dakika 13 katika Uwanja wa Upton Park jijini London.
Goli la kufutia machozi la West Ham limefungwa na James Tomkins