Michezo

Maneno ya Ronaldo baada ya Ubingwa wa Uefa 2017 (Picha)

Mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo wikiendi hii alikuwa na kibarua kizito katika mji wa Cardiff  pale ambapo timu yake ilipo ikabili kibibi cha torino Juventus ya Italia.

Wachezaji wa klabu ya Real Madrid wakishangilia ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya

Mara  baada ya kukisaidia kikosi cha kocha  Zinedine Zidane’ kutwaa kombe la klabu bingwa  barani Ulaya huku akitupia magoli mawili kati ya manne waliofunga katika mchezo huo.

Ronaldo alisema, “Namba iliyonyuma ya mgongo wangu haidanganyi”

“Hii ni moja ya kumbukumbu zangu bora katika tasnia yangu imezoeleka nikisikika nikisema hivi kila mwaka ,” alisema.

“Watu wamezoea kuni kukosoa kila siku ila najua kwa sababu namba haidanganyi.”

“Hii klabu ipo ndani ya moyo wangu na tunakwenda kuufurahia ushindi huu. Leo nisiku yaa historia ya kweli kwa  Real Madrid na mashabiki wote wa Madrid.”

Nae kiungo wa Real Madrid, Toni Kroos ambae kwa sasa ameshinda Champions League mara ya tatu akiwa na klabu ya Real pamoja na Bayern Munich,  alisema hapo ndipo thamani ya Ronaldo kwa Zidane’s inapo onekana .

“Siku tarajia, hili ni kama swala ambalo aliwezekani kutetea ubingwa huu, ni vigumu sana kushinda taji hili kwa mara nyingine nfululizo,”.

“Kila mtu anafahamu kuwa Cristiano ni muhimu. Kama timu tulicheza vizuri katika hatua ya robo fainali, nusu fainali na fainali lakini uanapo mtu wa kuhakikisha mnafunga magoli na yeye aliweza kufanya hivyo. alisema Toni Kroos.

 

Mchezaji Cristiano Ronaldo akitangazwa kuwa  man of the match , na Kocha wake wazamani ” Sir Alex Ferguson , huku mchezaji huyo akiwa na mtoto wake

Magoli aliyofunga katika kila kipindi cha mchezo yanamfanya  mreno huyo kufikisha jumla ya magoli 105 hii ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo klabu ya AC Milan mwaka 1990 baada ya kushinda na kutetea tena ubingwa.

Juventus ambayo ilionekana kufanya vizuri katika dakika 45 za kipindi cha kwanza,  Ronaldo alifungua lango la timu pinzani kwa kushinda goli la kwanza kwa upande wa Madrid kabla ya mchezaji wa Juve, Mario Mandzukic’s kuisawazishia timu yake.

Mabingwa wa klabu bingwa barani Ulaya klabu ya Real Madrid wakishangilia ubingwa wao baada ya kumngu Juventus kwa jumla ya magoli 4 kwa 1

Lakini Real  walikuja kwa kasi kupitia wachezaji wake  Casemiro, Ronaldo pamoja na  Marco Asensio  nakuifanya klabu hiyo kujinyakulia taji lake la 12 michuano ya Ulaya na latatu katika misimu minne

Ronaldo ndie mchezaji ambae amefunga angalau mara mbili katika mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya hatua ya robo fainali magoli (20), nusu fainali (13)  na fainali (4)  kuliko yeyote  .

Mchezaji huyu ameshinda mataji manne ya  klabu bingwa barani ulaya  na kwa sasa ameshinda zaidi ya magoli 11  katika mashindano haya  na kumshinda mpinzani wake wa karibu  Barcelona  Lionel Messi.

Picha zifuatazo ni Mapokezi ya klabu ya Real Madrid mbele ya mashabiki wao nchini Hispania

BY HAMZA  FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents