Michezo
Manuel Pellegrini kulipwa mkwanja mrefu zaidi West Ham
Manuel Pellegrini anatarajiwa kuwa kocha wa West Ham anaelipwa fedha nyingi kuwahi kutokea kwenye historia ya klabu hiyo mara baada atakapoingia kandarasi rasmi saa 48 zijazo.
Kocha, Pellegrini anatarajiwa kukusanya kitita kizito zaidi ya paundi milioni 16 aliyokuwa akilipwa kwa mwaka kwenye ligi ya China.
Duru za habari zinaeleza kuwa Mwanasheria wa meneja huyo upo kwenye hatua za mwisho kuhakikisha mambo yanakwenda sawa ndani ya klabu ya, West Ham ili kocha huyo mwenye umri wa miaka 64 aliyeachana na timu ya Hebei China anafanikiwa kwenye dili hilo.