Michezo

Manula wa Simba aukacha ukapera

Idadi ya wachezaji soka makapera inazidi kupungua. Golikipa wa klabu ya soka ya Simba, Aishi Salum Manula amejiondoa mwenyewe katika orodha hiyo.

Mchezaji huyo amefanikiwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu ajulikanaye kama Aisha.

Manula hakuweza kusafiri na kikosi cha Simba katika mashindano ya kombe la Mapinduzi yanayoendelea huko visiwani Zanzibar kwa ajili ya kukamilisha shughuli za ndoa hiyo.

Bongo5 tunawatakia ndoa yenye kudumu na amani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents