Habari

Maproducer wawili wakubwa jijini Arusha waingia katika beef zito

Samtimber

Maproducer wawili wakubwa jijini Arusha, Samtimber wa Fnouk Music Studios na Nisher wa Nisher Entertainment wameingia kwenye beef baada ya Samtimber kudai kuwa Nisher amekuwa akimletea dharau.

Akiongea na Bongo5, Samtimber amesema Nisher amekuwa akienda kwenye studio yake wakati akirekodi wasanii na kuanza kumkejeli kuwa anatengeneza ‘Bongo Flava’ na hawezi kufanya mixing.

Nisher

Samtimber ambaye alitengeneza track ya Fid Q na Lord Eyez, Neno, amesema hivi karibuni alirekodi wimbo wa kundi moja la Arusha ambao walienda kwa Nisher ili awafanyie video.

Nisher ambaye amefanya video kadhaa za wasanii wa Arusha ikiwemo Sijutii ya Joh Makini, anadaiwa kukataa kufanya video hiyo kwa madai kuwa ni wimbo wenye mixing mbovu.

Jana kupitia Facebook, Samtimber aliandika:

SIPENDI WANAUME WENYE TABIA ZA KIKE KAMA HUYU CHOKO ANAYEJIITA NISHER.NAMCHANA LEO LIVE NA TABIA ZAKE ZA KIKE KUPONDA KAZI ZA WENZAKE NA KUJIFANYA YE ANAJUA KILA KITU.WAKATI KAANZA JUZI NA KATUKUTA KWENYE GAME.MEN HUWEZI KUSHNDANA NA MIMI WALA M2 YOYOTE ALIYEKUTANGULIA C VIDEO MPAKA AUDIO.MADHARAU YAKO PELEKA KWENU KWANI MI C KULA KULALA KAMA WEWE NATAFUTA MAISHA YANGU MWENYEWE.SO NAKWAMBIA KABISA WE BADO XANA C AUDIO MPAKA VIDEO NA HUNA HEAT SONG YOYOTE.FANYA YAKO USIFATE YA WA2.

Juhudi za kumpata Nisher ili azungumzee kwa upande wake zinaendelea.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents