Muziki

Mara ooh wasanii badilikeni, wakisikia kuna video chafu imesambaa wanasaka makoneksheni – Content ya Joh Makini

Msanii wa muziki wa hip hop Joh Makini ameachia wimbo wake mpya uitwao ‘Maudhui. Audio ya wimbo huyo imeandaliwa na producer Bobo ndani ya  Switch Records na kufanyiwa mixing na mastering na Mixing na Chizan Brain.

 

Rapa huyo wa Kundi la Weusi amezungumzia jinsi watu walivyo-busy na mambo yasio kuwa na msingi na kuacha mambo ya msingi.

Wimbo huyo mpya ameuachia kipindi ambacho baadhi ya wasanii wamekuwa hawaachii ngoma bila kutafuta kiki ambayo inafanya azungumziwe kwanza kabla ya kuachia project mpya.

Joh katika wimbo huo pia amezungumzia namna wasanii wachanga wenye vipaji wanavyoapa wakati mgumu wa kutoka kimuziki licha ya kufanya kazi nzuri.

Je una maoni gani juu ya wimbo huu ?.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents