Michezo
Maradona amfananisha Louis van Gaal na shetani kwa kutompa nafasi Falcao
Wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Bogota, Colombia kupigia kampeni ya mechi ya hisani, nyota wa zamani wa Argentina, Diego Maradona alimkosoa kocha wa Manchester United Van Gaal kwa namna anavyomtendea Falcao.
Mcolombia huyo alikuja United akiwa na rekodi nzuri ya kufunga magoli, miezi nane baadaye, amejikuta akifunga magoli manne kwenye klabu hiyo.
Falcao amekuwa kwenye benchi kwenye mechi tano na hivyo kumkera Maradona.
Akizungumza na waandishi wa habari na kuulizwa kuhusu anavyomchukulia mholanzi huyo anavyomchukulia Falcao, Maradona alisema, “Van Gaal, si mtu mzuri, Van Gaal yuko karibu na shetani kuliko kitu chochote.”