Burudani

Marco Chali yupo chimbo kuandaa album yake

Marco Chali ameadimika kwa kiasi kikubwa si tu katika mzunguko wa nyimbo mpya, bali hata yeye mwenyewe haonekani kabisa siku hizi.

Kunani? Mara ya mwisho nilimpigia simu kutaka kujua nini anachokiandaa, alikataa katakata kuongea chochote akidai kuwa muda wa kufanya hivyo haujafika.

Na sasa huenda tukawa tumepata jibu la kwanini amekuwa kimya na nini anachokifanya. Rapper Izzo Bizness ndiye aliyetoa siri kwa kudai kuwa producer huyo wa MJ Records anaanda album yake.

“Marco alinipigia simu, wiki kama tatu zilizopita na aliniambia anafanya album yake so kuna track moja amenipa, kwahiyo aliniambia nijipange, so project na Marco very soon,” Izzo alimuambia Lil Ommy wa Times FM kupitia show yake ya The Playlist.

Sikiliza mahojiano hayo chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents