Habari

MAREKANI: Leo ndio kumbukumbu ya miaka 18 ya shambulio la septemba 11, lililosababisha vifo vya watu 3000 – Video

MAREKANI: Leo ndio kumbukumbu ya miaka 18 ya shambulio la septemba 11, lililosababisha vifo vya watu 3000 - Video

Septemba 11, 2001 ni tarehe inayokumbukwa kwa shambulizi baya kuwahi kufanyika Marekani na kusababisha vifo vya watu takribani 3,000 na kujeruhi wengine 6,000 baada ya kundi la kigaidi la Al-Qaeda kuteka ndege nne.


Kundi hilo likiongozwa na Osama bin Laden waliziteka ndege hizo ambapo ndege ya kwanza iliyokuwa ikitokea Boston, ililazwa kwenye mnara wa Kaskazini wa Kituo cha Biashara Ulimwenguni jijini New York.Ndege ya pili, pia kutoka Boston, iligonga mnara wa Kusini dakika 17 baada ya ile ya kwanza. Ndege ya tatu ikitoka Uwanja wa Ndege wa Dulles iligonga upande wa Kusini Magharibi wa Pentagon.

Ndege ya nne kutoka Newark, New Jersey, iligonga karibu na Shanksville mashambani mwa Pennsylvania baada ya abiria kupata habari ya matukio na kujaribu kuwashambulia watekaji.


Tangu shambulio hilo kutokea, Marekani walikuwa wakimsaka kiongozi wa kundi hilo Osama Bin Laden na kufanikiwa kumuua May 2, 2011 na Marekani imekuwa ikipunguza vikosi vyake nchini Afghanistan tangu Osama alipouawa.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents