Habari

MAREKANI: Mwalimu aliyembaka mwanafunzi wake na kisha kufunga naye ndoa afariki dunia

Aliyekuwa mwalimu katika jimbo la Washington ambaye uhusiano wake na mwanafunzi ulifanya akafungwa gerezani na kukashifiwa kote duniani ameaga dunia kwa ugonjwa wa saratani akiwa na umri wa miaka 58.

Mary Kay Letourneau alipatikana na hatia ya mauaji ya daraja la pili ya kubaka mtoto mwaka 1997 baada ya kupata ujauzito na Vili Fualaau alipokuwa na umri wa 12 au 13 na yeye alikuwa na umri wa miaka 34.

Alijifungua mtoto wao wa pili akiwa gerezani 1998.

Baada ya kumaliza kifungo chake, wanandoa hao walioana 2005, hatahivyo, walitengana baada ya miaka 12.

Waliki wa Bi. Letourneau, David Gehrke ameviambia vyombo vya habari vya Marekani kwamba Bi. Letourneau amekufa nyumbani kwake akiwa na watoto wake na Bwana Fualaau.

Bi. Letourneau alikuwa mama aliyeolewa na watoto wanne wanaoishi Seattle alipoanza uhusiano na mwanafunzi wake wa darasa la sita.

Awali, alihudumia kifungo cha miezi kadhaa tu gerezani lakini baada ya kuachiliwa huru alipatikana akifanya ngono tena na kijana huyo huyo mdogo.

Mama huyo aliyekuwa mwalimu alirejeshwa tena gerezani na kuhudumia kifungo cha miaka saba. Binti zake wawili aliopata na kijana Fualaau awali walitunzwa na familia ya mume wake.

Inasemekana kwamba mama huyo amekuwa mgonjwa kwa miezi sita kabla ya kutokea kwa kifo chake.

Mama huyo alikuwa mkatoliki na ni binti ya aliyekuwa mbunge wa Republican, John G. Schmitz. Lakini taaluma ya baba yake kisiasa ilifikia ukingoni baada ya kujitokeza kwa kashfa ya kwamba alikuwa na watoto wawili nje ya ndoa.

Chanzo BBC.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents