Michezo
Marin Cilic ashindwa kutamba mbele ya Guido Pella michuano ya Wimbledon
Mchezaji tennis, Marin Cilic ameyaaga mashindano ya Wimbledon leo siku ya Alhamisi baada ya kushindwa kuvumilia kipigo kutoka kwa Muargentina, Guido Pella.
Cilic ambaye alitarajiwa makubwa kwenye mashindano haya ya Wimbledon baada ya kushinda taji la Fever Tree Championships huko Queen’s Club ameshindwa kuepukana na kichapo hicho.
Mbosnia huyo amekubali kipicha jumla ya seti 3-6 1-6 6-4 7-6 (7-3) 7-5 kutoka kwa Guido Pella anayeshika nafasi ya 82 kwenye viwango vya ubora wa mchezo huo duniani.