Mario Mandžukić afuata nyayo za Wahispanyola Gerrad Pique pamoja na David Silva
Mario Mandžukić afuata nyayo za Wahispanyola Gerrad Pique pamoja na David Silva
Hii imekuwa ni wiki ya wachezaji kutundika daluga baada ya Gerrad Pique kutoka nchini Uhispania kuamua kutundika daluga ikafuata zamu ya Mhispania mwingine David Silva kutangaza kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa ya Uhispania leo imekuwa zamu ya Mcroatia huyu si mwingine bali ni Mario Mandžukić .
Mandžukić ameandika waraka kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa anaamua kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa ya Croatia,Mario ameongea mengi sana kuhusiana na mafanikio aliyoyapa katika taifa lake kupitia soka lakini pia kuweza kukutana na wachezaji mbalimbali.
Na haya ndio maneno yake:-
Mario Mandžukić alizaliwa miaka 32 iliyopita,May 21 ya mwaka 1982 katika nchi ya Croatia na amefanikiwa kuvitumikia zaidi ya vilabu 7 katika karia yake ya mpira vikiwemo Bayern Munich,Atletico Madrid na kwa sasa akiitumikia Juventus.
Lakini pia katika timu yake ya taifa ya wakubwa alifanikiwa kujiunga nayo mwaka 2007 akicheza michezo 89 na akiifungia magoli 33 akiwa mfungaji wa pili wa muda wote katika taifa hilo mwenye magoli mengi akizidiwa na mkongwe Dvor Suker mwenye magoli 45.
By Ally Juma.