Michezo

Mashabiki wa Chelsea wamzomea Hazard

Baada ya Chelsea kuondoshwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya na timu ya PSG kwa jumla ya magoli 4-2, Hazard ameingia kwenye mzozo na mashabiki wa timu hiyo baada ya kubadilishana jezi na Di Maria.

suspicious-shirt-s_2733121a

Hazard alijikuta akizomewa na mashabiki wa timu yake ya Chelsea baada ya kubadilishana jezi na Di Maria kipindi cha mapumziko wakati huo timu hizo zikiwa zimefungana goli moja kwa moja, kipindi cha pili Ibrahimovic aliifungia PSG goli la pili na la ushindi.

Kocha wa Chelsea, Guus Hiddink amesema,”Ndio, walikuwa sahihi kufanya walichokuwa wanakifikiria. Siyo mbaya kuonyesha hisia zako.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents