Burudani

Mashabiki wa Nicki Minaj wafurahia uamuzi wake wa kuchagua muziki na kuitosa American Idol

Juzi rapper wa kike ambaye mwaka huu alipata cheo kingine cha ujaji katika shindano la kusaka vipaji ‘American Idol’ alitangaza kujiondoa katika meza ya ujaji kwa msimu ujao, uamuzi ambao umepewa baraka zote na mashabiki wa muziki wake.

nicki-minaj-

Habari za uamuzi huo wa Onika Tanya Maraj maarufu kama Nicki Minaj zilijulikana wiki hii (May 30) sambamba na uamuzi kama huo wa aliyekuwa jaji mwenzake Mariah Carey ambaye pia alisema ameamua kurudisha nguvu zake katika muziki.

Hizi ni kati ya tweets za walioonekana kufurahishwa na uamuzi wa Minaj,

-“@NICKIMINAJ IIIII AAMMM READDDYY FOR THE F—ING MUUSSSSIIICCCCCCCCCCCCCC. YOU HAVE NO IIIIDDDEEEEAAAAAAHHHHHH.”
– “Yass @AmericanIdol thank you for letting @NICKIMINAJ B in the show,”
– “We that Barbs appreciate it and wanna say … Thank You.”

Katika msimu wa 12 wa American Idol ulioisha, Nicki Minaj na Mariah Carey walithibitisha usemi wa mafahari wawili hawakai zizi moja, baada ya kugombana kwa maneno na vitisho toka mwanzo wa shindano hadi mwisho. Of course drama huongeza ladha ya tukio hivyo watakumbukwa kwa drama zilizo make headlines katika American Idol season 12.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents