Michezo

Mashabiki wa soka nchini Korea waomba walipwe fidia baada ya Ronaldo kutoingia uwanjani na kukaa benchi haliyakuwa walienda kumuona yeye

Mashabiki wa soka nchini Korea waomba walipwe fidia baada ya Ronaldo kutoingia uwanjani na kukaa benchi haliyakuwa walienda kumuona yeye

Mashabiki wenye hasira wa Korea Kusini wanataka walipwe fidia baada ya Cristiano Ronaldo kushindwa kuingia uwanjani wakati wa mchezo wa kirafiki wa kabla ya msimu dhidi ya Juventus. Nyota huyo wa Ureno alikuwa amesaini mkataba wa kucheza dakika 45 wakati mechi dhdi ya timu hiyo ya Ligi K ya nyota wote ilipotangazwa , wanasema waandalizi, lakini alikaa kwenye benchi nje ya uwanja.

Mashabiki walijawa na ghadhabu wakati aliposhindwa kuonyesha ishara yoyote ya kuingia uwanjani, hata wakaanza kushangilia kwa kupaza sauti wakilitaja jina la hasimu wake Lionel Messi.

Kwa mujibu wa BBC. Baadhi ya mashabiki sasa wamekwenda hadi kwenye kampuni ya sheria mjini, inayofahamika kama Myungan kuwasilisha mashtaka.

Wanataka walipwe fidia ya won 70,000 (£48.50; $59) kwa kila tiketi , na milioni 1 ya fidia kwa kila mmoja kutokana na kile wanachokitaja kuwa “kuathirika kiakili “.

“Kwa kawaida katika hali kama hii mlalamikaji hulipwa gharama ya tiketi, lakini swala hili ninalichukulia kama swala la kipekee kwasababu kampuni , kupitia matangazo ya uongo, iliwalaghai mashabiki wa nyota huyo,” alisema wakili kutoka kampuni ya mawakili katika mazungumzo na shirika la habari la Reuters.

“Kwa upande wa tatizo la kuathirika kiakili , ningependa kusema kwamba baadhi yao ni mashabiki sugu, mashabiki sugu kabisa. Kwa hiyo kwao ni uchungu mkubwa kwasababu wanampenda Ronaldo na wanataka kumlinda, lakini hawawezi, kutokana na hali halisi ,” aliongeza.

Ronaldo alitumia muda wake wote wa mechi kukaa kwenye benchi ya wa wachezaji wa ziadaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRonaldo alitumia muda wake wote wa mechi kukaa kwenye benchi ya wa wachezaji wa ziada

“Kwa sasa tuna walalamikaji ambao waliishtaki kampuni , lakini nimekuwa nikipokea simu nyingi leo na ninadhani ni zaidi ya simu 60,000 .”

Robin Chang, Mkurugenzi mkuuu wa The Fasta, wakala wa Korea walioandaa mechi hiyo aliangua kilio mbele ya waandishi wa habari wa kampuni ya SBS na kuthibitisha kuwa mkataba ulieleza wazi kuwa Ronaldo angecheza kwa dakika 45.

Hata hivyo, Bi Chang alibaini tu kwamba mchezaji huyo wa miaka 34 hatacheza mechi dakika 10 tu baada ya kipindi cha pili.

“Nilipoenda kujaribu kuzungumza na (Pavel) Nedved, naibu rais wa Juventus, kile alichoniambia ni kwamba ‘pia mimi ningetamani Ronaldo acheze , lakini hataki kufanya hivyo . Samahani , hakuna ninaloweza kulifanya .’ Nilisikitika sana ,” alisema.

Shirika la soka la Korea Kusini Korea , K League, limesema kuwa barua ya kupinga tayari imetumwa kwa Ligi ya Championi ya Italia kwa kukiuka mkataba. Mashabiki wengi wamekuwa wakielezea hasira yao shisi ya Ronaldo kwenye mitandao ya habari ya kijamii.

“Amesaliti mashabiki 60,000 na kutudharau,” alisema mmoja wa mashabiki waliokuja kutazma mechi hiyo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents