Yafahamu masharti aliyopewa Mario Balotelli baada ya kujiunga na AC Milan
Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli aliyekuwa akiichezea Liverpool ya Uingereza sasa amejiunga na klabu ya AC Milan ya Italia kwa mkopo wa muda mrefu.
Balotelli alijiunga na AC Milan ikiwa ni msimu mmoja umepita toka ahamie Liverpool akitokea klabu ya AC Milan.
Kuna taarifa mpya zimetoka kuhusu mkataba wake na vipengele vilivyopo ambapo imethibitishwa kuwa kuna kipengele kinachomzuia kuweka style za nywele za ajabu, kuvuta sigara ili kulinda afya yake, afike mazoezini kwa wakati, kunywa pombe na kwenda club bila mpangilio.
Gazeti la dello Sport linaeleza kuwa afisa mtendaji mkuu wa klabu ya AC Milan, Adriano Galliani ameeleza kuhusiana na kipengele hicho kuwemo kwenye mkataba ni kutokana na Balotelli kuwahi kukutwa mara nyingi na makosa mbalimbali likiwemo la kukutwa na mhudumu wa treni akivuta sigara katika choo cha treni.
Haya chini ni baadhi ya makosa ambayo Balotelli amewahi kufanya na faini alizolipa: