Michezo
Mashindano ya Magari yaanza Dar
Leo saa moja asubuhi magari 22 yalianza mashindano yake katika viwanja vya Mlimani City, na kuzunguka hadi Bagamoyo ambapo watafanyia matengenezo ya muda kwa magari hayo katika sehemu moja inayoitwa Baobao kabla ya kuendelea na safari hiyo.
Magari hayo yatamaliza mashindano hayo saa kumi jioni na kisha siku ya kesho jumapili yataanza tena kwaajili ya kumtafuta mshindi, katika viwanja vya Mlimani City muda unaokadiriwa saa kumi .