Burudani

Masogange aachiwa huru, aukwepa mlango wa gereza kwa kulipa faini

Hatimaye mrembo Agnes Gerald maarufu kwa jina la Masogange ameachiwa huru katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kulipa faini ya kesi iliyokuwa inamkabili.

Masogange ambaye leo (Jumanne) alipatikana na hatia ya makosa mwawili ya kutumia dawa za kulevya.

Kosa la kwanza ni kutumia dawa za kulevya aina ya heroine, na la pili kutumia dawa za kulevya aina ya 0xazepam.

Mahakama hiyo ilimuhukumu mrembo huyo kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni 1.5 za kitanzania ambapo Masogange amefanikisha kulipa faini hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents