Michezo
Mastaa kibao washuhudia mechi kati ya Serena na Venus Williams
Mastaa kibao jana walijitokeza kushuhudia mchezo wa tennis ambapo Serena Williams alimshinda dada yake Venus kwenye michuano ya US Open.
Serena Williams aliyeipa mgongo camera akikumbatiwa na dada yake kiumri, Venus
Baada ya mchezo huo Serena alisema: She’s the toughest player I’ve ever played in my life.”
Mastaa hao ni pamoja na mgombea urais wa Marekani, Donald Trump aliyeungana na mke wake Melania, Oprah Winfrey na rafiki yake Gayle King pamoja na mhariri wa jarida la Vogue, Anna Wintour.
Wengine ni pamoja na Kim Kardashian na mdogo wake Kendall Jenner rappers, Nas na Kendrick Lamar, msanii wa soul, Gladys Knight na wengine.