Burudani
Mastaa wa Nigeria wafurika Port Harcourt kuhudhuria harusi ya Paul Okoye wa P-Square
Mastaa wa Nigeria pamoja na wanasiasa wamefurika kwenye mji tajiri kwa mafuta wa Port Harcourt kuhudhuria harusi ya kimila ya Paul Okoye na Anita Isama.
Ijumaa hii, uwanja wa ndege wa Lagos ulishuhudia abiria wengi waliokuwa wakielekea Port Harcourt kwenda harusi ya pacha huyo wa kundi la P-Square.
Harusi hiyo inafanyika leo Jumamosi mjini humo.