Burudani
Mastaa Wapamba Uzinduzi wa ‘Freedom For All’ ya Shaykaa (Video)
Mrembo Shaykaa ambaye amekuwa akionekana katika harakati za kusaidia watu wa chini pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira magumu, usiku wa jana katika hotel ya New Africa jijini Dar es salaam ameanza rasmi safari yake katika muziki. Muimbaji huyo akiwa na Heri Muziki pamoja na PaulĀ alizindua wimbo wake mpya uitwao Freedom For All ambapo mastaa mbalimbali walihudhuria uzinduzi huo.