Diamond Platnumz
Matapeli wanaodai kutoa mikopo bila riba wahack akaunti ya Diamond na kujipigia ‘promo’
Kundi la matapeli wanaojiita Saving Foundation leo wameihack akaunti za Facebook na Twitter za Diamond na kuandika ujumbe unaoonekana kama umeandikwa na Diamond.
Tumempigia simu na Diamond ambaye hakuwa na taarifa zozote kumuuliza kama ni yeye ndiye aliyeandika na amekanusha kuandika ujumbe huo.
Ujumbe huo kwenye akaunti ya Facebook ya Diamond unasomeka:
Naimani kuwa Serikali yetu ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania imeamua kuwasaidia watanzania masikini kidhat… fb.me/34VuPrEZl
— Diamond Platnumz (@diamondplatnumz) June 11, 2013
Matapeli hao pia wamewahi kutumia majina ya Zitto Kabwe na Ridhwan Kikwete kufanya utapeli huo.
Mtaalam mmoja wa masuala ya IT ameiambia Bongo5 kuwa matapeli hao wamejipanga na wana mtandao mkubwa.