Michezo
Matokea ya michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya iliyo pigwa February 23
Usiku wa February 23 iliendelea michuano ya klabu Bingwa barani Ulaya kwa klabu ya FC Barcelona ya Hispania ilikuwa imesafiri kutoka Hispania hadi London Uingereza kukutana na Arsenal katika mchezo wao wa kwanza hatua ya 16 bora.
Mchezo huo ulimalizika kwa Lionel Messi kuipa ushindi FC Barcelona wa goli 2-0, magoli ya Lionel Messi yaliofungwa dakika ya 71 na 83,.
Mchezo mwinigne wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ulikuwa, Bayern Munich ambayo imelazimisha sare ya 2-2 na wenyeji Juventus Uwanja wa Juve.
Paulo Dybala akishangilia baada ya kuipatia Juventus bao la kwanza
Bayern ilitangulia kwa mabao ya Thomas Muller dakika ya 43 na Arjen Robben dakika ya 55, kabla ya Paulo Dybala kuifungia Juve dakika ya 63 na Stefano Sturaro kusawazisha dakika ya 76.