Burudani
Matonya: Sasa hivi kila mwezi na ngoma mpya
Matonya hataki tena kukaa kimya muda mrefu bila kuachia wimbo mpya. Sasa amepanga kuachia ngoma kila mwezi.
Akiongea na E-News ya EATV msanii huyo amesema amesikia kilio cha mashabiki wake kuwa wanamiss kazi zake.
“Sasa hivi nipo kikazi zaidi, mwanzo nilikuwa nimetingwa na majukumu binafsi na shughuli za hapa na pale,” alisema.
“Nashukuru sasa hivi majukumu yamekaa vizuri, kwahiyo sasa hivi nipo kikazi zaidi. Nawakaribisha wote ambao wanataka kushirikiana na mimi kikazi. Na pia sasa hivi itakuwa ni bandika bandua, yaani nitakuwa natoa ngoma kila mwezi maana nasikia mashabiki wangu mtaani wamenimiss sana.”