Burudani

Maua Sama ataja sababu ya kutoachia video ya ‘Sisikii’

Maua Sama amefunguka sababu ya kushindwa kuachia video ya wimbo wake ‘Sisikii’.

Akiongea na kipindi cha Flavour Express cha Maisha FM ya Dodoma, muimbaji huyo ameitaja sababu ya kuchelewa ni video hiyo kuhitaji marekebisho makubwa ambayo yangempotezea muda zaidi.

“Muda ndio uliotutupa mkono halafu mwisho wa siku video ilikuwa inahitaji marekebisho mengi ambayo kimsingi isingeweza kutoka mapema, na mimi ingeweza kunigharimu gharama za video nzima na muda ulikuwa umeshakwenda wakati ambao nilikuwa natakiwa kutoka na wimbo mwingine,” amesema Maua.

Hitmaker huyo wa Main Chick, ametaja sababu ya kufanya kazi na Luffa badala ya Imma The Boy kama ilivyozoeleka kwa kusema, “Hata yeye mwenyewe alinishauri kubadilisha producer kwa sababu tulikuwa tunarekodi nyimbo na mwisho wa siku tuna sound the same, akaniambia ungebreak utafute producer mwingine nifanye naye. Mimi nikaona siyo vibaya hata uongozi wangu nao ukashauri nitafute producer mwingine, nimepata maproducer ambao kiukweli nafanya nao kazi kama hivyo Luffa na wengine”.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents