Michezo
Maurizio Sarri kurithi mikoba ya Antonio Conte mwishoni mwa juma hili
Meneja wa klabu ya Chelsea, Antonio Conte anatarajiwa kuachana na timu hiyo mwishoni mwa juma hili na nafasi ya kuchukuliwa na Maurizio Sarri kwaajili ya kuanza maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu nchini Uingereza.
Maurizio Sarri
The Blues ilikuwa na mpango wa kuachana na Conte tangu kati ya mwezi Mei na nafasi yake kuchukuliwa na Sarri aliyejkuwa meneja wa klabu ya Napoli.
Chelsea inatarajia kumtangaza rasmi kocha hiyo raia wa Italia Mwenye umri wa miaka 59 mwishoni mwa juma hili huku Sarri akiwa meneja wa 12 ndani ya Stamford Bridge tangu Roman Abramovich kuichukua klabu hiyo mwaka 2003.