Burudani
Mauzo ya tiketi za pambano la Mayweather Jumamosi hii yadoda
Mauzo ya tiketi za pambano la Floyd Mayweather Jr na Andre Berto Jumamosi hii yamedoda.
Tofauti na pambano lake lililopita dhidi ya Manny Pacquiao miezi minne iliyopita, tiketi za pambano hilo zimeendelea kupatikana kirahisi.
Mayweather aliingiza zaidi ya dola milioni 200 kwenye pambano na Pacquiao.
Katika pambano la Jumamosi hii, Mayweather ataingia dola milioni 32.
Pambano hilo litachezwa kwenye ukumbi wa MGM Grand Garden Arena.
Berto ameshindwa mapambano matatu kati ya sita aliyopigana mwishoni.