Habari
Mbakaji sugu ajinyonga kwa blanketi akiwa gerezani Afrika Kusini
Mwanamume anayetuhumiwa kuwa mbakaji sugu nchini Afrika Kusini ,Sifiso Makhubo, amekutwa akiwa amefariki katika chumba chake gerezani.
BBC Swahili imeripoti kuwa Sifiso Makhubo, alikuwa anakabiliwa na mashtaka 122 ikiwa ni pamoja na mauaji na ubakaji . Makhubo alikutwa amejinyonga kwa kutumia blanketi katika chumba chake cha gerezani.
Makhubo anatuhumiwa kwa kuwabaka watoto 35 na wanawake wawili, kati ya Januari mwaka 2006 na Februari 2011.
Hadi sasa uchunguzi uliofanywa wa DNA katika waathiriwa waliodai kubakwa naye, ulithibitisha kuwa yeye ndiye alikuwa mbakaji.
SOURCE: BBC SWAHILI