Michezo

Mbao FC yamsajili kocha wa Lipuli

Klabu ya soka ya Mbao FC, imetangaza rasmi kumsajili kocha Amri Said.

Kocha huyo amesaini mkataba wa miaka minne ambao utamalizika msimu wa mwaka 2021/2022. Makubaliano hayo yamefikiwa katika ofisi za makao makuu ya wadhamini wa Mbao, GF Trucks &Equipment ltd zilizopo Vingunguti jijini Dar es salaam.

Msimu uliopita Amri Said alikuwa akiifundisha Lipuli FC huku msaidizi wake akiwa Selemani Matola na kuisaidia timu hiyo ikimaliza ligi kuu ikiwa kwenye nafasi ya saba.

Wakati huo huo Mbao imenusurika kushuka daraja msimu ulioisha ikiwa nafasi ya 14 na huku ikiambulia alama 29.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents