Michezo

Mbappe kuweka rekodi ya karne, atakaye fikia dau lake la usajili awe kidume kweli, si Neymar wala Ronaldo 

Real Madrid wanaangalia uwezekano wa kutoa malipo makubwa kuwahi kushuhudiwa ya pauni milioni 340 kwa ajili ya mchezahi wa safu ya mashambulio wa Paris St Germain mwenye umri wa miaka 20 Kylian Mbappe. (Le Parisien via Calciomercato)

Real Madrid wanaangalia uwezekano wa kutoa malipo makubwa kuwahi kushuhudiwa kumchukua Kylian Mbappe

Huo utakuwa usajili mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya soka kwa kuwa anayeshikilia rekodi ni Neymar ambaye alisajiliwa kwa dau wa pauni milioni 200 wakati Ronaldo akienda Juventus kwa pauni milioni 105.

Cristiano Ronaldo hatalipishwa faini na Juventus kutokana na mienendo aliyoonyesha baada ya kutolewa uwanjani na badala yake kuwekwa mchezaji wa ziada katika mchezo wa pili.

Ingawa mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 34, atatarajiwa kuomba msamaha kwa wachezaji wenzake. (Gazzetta dello Sport, in Italian)Cristiano Ronaldo anatarajiwa kuomba msamaha

Cristiano Ronaldo anatarajiwa kuomba msamaha

Barcelona wanamtaka mshambuliaji wa timu ya Salzburg mwenye umri wa miaka 19 Erling Braut Haaland kama mtu atakayechukua nafasi ya Luis Suarez mwenye umri wa miaka 32, lakini wanasitasita kuafiki kiwango cha thamani ya mchezaji huyo wa klabu ya Austria cha pauni milioni 85. (ESPN)

Rais wa klabu ya Napoli Aurelio de Laurentiis amepokea Euro milioni 560 kwa ajili ya Ligi ya klabu ya Serie A kutoka Qatar huku mashabiki wakipinga na wachezaji wakigoma . (Mail)Nemanja Matic anataka kuondoka Manchester United ikiwezekana mwezi Januari

Nemanja Matic anataka kuondoka Manchester United ikiwezekana mwezi Januari

Tottenham wanatarajia kumchukua mshambuliaji wa kati wa timu ya Roma ya Italia Lorenzo Pellegrini, mwenye umri wa miaka 23, kama mtu anayeweza kuchukua nafasi ya Christian Eriksen. (Football Italia)

Nemanja Matic anataka kuondoka Manchester United, ikiwezekana mwezi Januari, huku kiungo huyo wa kati Mserbia mwenye umri wa miaka 31 akitarajiwa kwenda Italia. (telegraph)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents