Michezo

Mbeya City yaweka hadharani jezi zake mpya (Picha)

Klabu ya Mbeya City imeweka hadharani jezi zake mpya zitakazo tumika kwaajili ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara huku zikionekana kuwa na chata ya mdhamini wake mbele ya uzi huo.

Mwenyekiti Mussa Mapunda na Fadhili Nsemwa (Afisa Masoko SportsMaster) wakizindua rasmi jezi na vifaa vya msimu huu.

Bakari Masoud na Owen Chaima wakiwa wamevalia jezi ya ugenini na jezi ya mazoezi.

Mwanamitindo Salma akipita mbele ya waalikwa na Jaketi mpya ya klabu ya Mbeya City Fc. Jaketi hii inapatikana pia madukani.

Usungilo Hall/Mbeya. Uzinduzi wa Jezi.

Mwanamitindo Mourine aliyekua Miss Nyanda za Juu Kusini na wenzake wakipita na Jezi ya mashabiki ya kike iliyozinduliwa jana.

 

Mrisho Ngassa na John Kabanda wakipita mbele ya umma kuonesha jezi mpya ya nyumbani ya msimu huu.

By Hamza fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents