Michezo
Mbwana Samatta aingia orodha ya 3 bora ya CAF
Mshambuliaji wa Taifa Stars ya Tanzania na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mbwana Samatta ametangazwa katika orodha ya wachezaji watatu bora na shirikisho la soka la Afrika CAF wanaocheza soka barani Afrika.
Samatta anashindana na wachezaji wengine wawili Baghdad Boundjah wa Algeria na Etoile du Sahel na Kipa machachari wa TP Mazembe ya DR Congo Robert Kidiaba.
Mshindi atachaguliwa na makocha wa timu za taifa na kutangazwa katika dhifa maalum Januari tarehe 7 mwakani.
CAF ilikuwa imewataja wachezaji 37 katika orodha ya awali lakini wakachuja hadi 10 mwezi uliopita.