Uncategorized

Mchekeshaji nchini Ukraine ashinda Urais

Msanii wa vichekesho nchini Ukraine, Volodymyr Zelensky amepata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa urais, kutokana na kura zilizopigwa.

Kura hizo zimempa nafasi mwanasiasa mpya ambaye amechaguliwa kwa kuungwa mkono na zaidi ya asilimia 70.

Bwana Zelensky mwenye umri wa miaka 41, ameweza kumtoa madarakani rais Petro Poroshenko ambaye amekubali kushindwa.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Matokeo ya sasa yanaonekana kuwa ni pigo kubwa kwa bwana Poroshenko na kukataliwa kuanzishwa kwa Ukraine mpya.

“Sitawaangusha ,” Bwana Zelensky aliwaambia waliomuunga mkono wakati wa sherehe za kujipongeza.

Aliongeza kusema “Sijawa rais bado lakini kama raia wa Ukraine, ninaweza kuwaambia nchi zote za Kisovieti kuwa watuangalie sisi, Kila kitu kinawezekana !”J

“Kama kura ziko sawa, basi atakuwa amechaguliwa kuongoza kwa kipindi cha miaka mitano”. Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa hapo baadae.

Zelensky anajulikana kwa umahiri wa ucheshi wake kama muigizaji nyota wa mfululizo wa filamu ya satirical katika television ambapo anaigiza kama rais wa Ukraine.

Rais ana mamlaka makubwa katika upande wa usalama, jeshi na sera za kigeni katika nchi hiyo.

Presentational grey line

Aibu ya Poroshenko

Petro Poroshenko
Image captionPetro Poroshenko

Uchaguzi wa Ukraine unaangalia mwanasiasa mwenye ujuzi wa miaka mitano katika urais na katika wasifu wa mchekeshaji aliyeshinda hana ujuzi zaidi ya karatasi tu.

Watu wengi wamempigia kura Volodymyr Zelensky ambapo ni aibu kubwa kwa Petro Poroshenko.

Wagombea thelathini na saba waliondolewa kwenye karatasi ya uchaguzi kutoka pande zote za kwanza na bado rais alichukua kura zaidi ya asilimia 9 wakati huu na bwana Zelensky alipata karibu asilimia 45

Hii inaonyesha kuwa kura nyingi zilipigwa kwa ajili na timu yake ya kampeni iliyokuwa inasheherekea.

Aidha ni ngumu kuona hisia hizo kudumu kwa muda. Kazi kubwa inakuja pale utekelezaji unapoanza .

Ni jambo moja kuwa na wazo lakini jambo lingine ni utekelezaji.

Presentational grey line

Kura zilimpa ushindi wa urais bwana Poroshenko, mwaka 2014 kwa asilimia 25 za kura.

“Matokeo ya urais yanatuacha njia panda”, alisema baada ya kura kutangazwa.

Bwana Poroshenko aliongeza, “Nitatoka madarakani lakini sitaacha siasa.”

Volodymyr Zelensky ni nani?

Zelensky amekuwa akicheza mchezo wa kuigiza inayoitwa ‘Servant of the People ‘ ambapo kwa bahati tu akawa muigizaji anayetaka kuwa rais wa Ukrainne.

Anacheza kama mwalimu ambaye aliyechaguliwa baaada ya kufukuzwa kwa kosa la rushwa kusambaa katika mitando ya kijamii.

Aligombea nafasi ya urais kwa jina la chama cha siasa ambacho ni sawa na kipindi chake cha televisheni.

Volodymyr Zelensky
Image captionVolodymyr Zelensky amehaidi kupambana na rushwa

Akiwa hana uzoefu wowote wa siasa ,wkampeni za Zelensky ziliangazia utofauti wake na wagombea wengine badala ya mawazo ya sera.

Awamu ya kwanza alishinda kwa asilimia zaidi ya 30 za kura ambapo zilikuwa ni mara mbili ya mpinzani wake Poroshenko ambaye alikuwa na asilimia 15.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents