Michezo
Mchezaji aliyetua Simba amtesa Kaseja
Shija Mkina amemtesa kipa wa Simba Juma Kaseja katika mazoezi ya timu ya Simba yanayofanyika kwenye uwanja wa Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam. Shija aliesajiliwa na Simba kutoka Kagera Sugar alifunga mabao manne maridadi Kaseja katika mazoezi ya juzi alhamisi yaliyokuwa chini ya kocha mkuu msaidizi Syller Said Mzirai.
Mkina ambaye ana uwezo wa kucheza hata nafasi ya kiungo pamoja na ushambuliaji alionekana kufanya vizuri katika mazoezi hayo na hata kutishia nafasi za nyota wa timu hiyo Mussa Hassan Mgosi na Emmanuel Okwi.
Habari nzuri kwa Mkina ni kuwa Mgosi atakuwa nje ya uwanja kwa siku tano hivyo kumpa nafasi kuzidi kutamba mazoezini.
Mgosi atakuwa akitibiwa Hospitali ya Aga Khan kwa muda wa siku tano.