Burudani

Mchezaji wa Mbao FC U 20, Ismail Mrisho afariki uwanjani

Kinda wa Mbao FC ya Mwanza, Ismail Mrisho Khalfan amefariki dunia Jumapili ya jana baada ya kuanguka uwanjani alipogongana na beki wa Mwadui FC katika michuano ya Ligi ya Vijana U20 inayoendelea.
dv2a0262
Akiwa huduma ya kwanza baada ya kuanguka

Mechi hiyo ilipigwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba na juhudi kubwa zilifanyika kuokoa maisha ya kinda huyo, lakini haikuwezekana.
mchezaji
Akitolewa nje baada ya kuanguka

“Inaonekana alishafariki dunia pale uwanjani, tulifanya juhudi kubwa mimi na wenzangu. Tulisaidiana na watu wengine pia waliokuwa uwanjani, lakini ilionekana hakukuwa na majibu mazuri,” alisema mmoja wa madaktari waliojaribu kuokoa maisha ya kijana huyo.

Mwenyezi Mungu Amrehemu.

Source: Michuzi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents