Michezo

Mchezaji wa Tottenham hatiani kwa kupanda jukwaani, Kwenda kupigana na shabiki baada ya kutolewa FA, Mourinho amtetea – Video

Mchezaji wa Tottenham hatiani kwa kupanda jukwaani, Kwenda kupigana na shabiki baada ya kutolewa FA, Mourinho amtetea - Video

Moja ya tukio la kushangaza lililotokea katika mchezo wa spurs dhidi ya Norwich ni pale beki wa Tottenhma Eric Dier kupanda kwenye jukwaa la mashabiki na kwenda kumshambulia shabiki alikuwa akipiga kelele za kumtuka  kaka yake, ambaye alikuwa amekaa karibu naye.

Inaelezwa kuwa Kaka yalke Dier alikuwa anajaribu kumtuliza shabiki huyo ambaye alikuwa akitoa kauli mbaya baada ya Tottenham kutolewa kwenye michuano ya FA.

 Video nyingi zilionyesha Dier akiacha mlango wa kutokea wachezaji na kupanda jukwaani ROWS 20 ambayo huwa wanakaa ndugu na marafiki au watu wa karibu wa wachezaji mbalimbali pale alipoona kaka yake anashambuliwa kwa kauli mbaya na shabiki huyo, Dier alisikika akipiga kelele akisema “Huyo ni ndugu yangu” baada ya kuzuiliwa na baadhi ya amshabiki asifanye fujo au kumpiga shabiki huyo.

Huenda Dier akakutana na adhabu ya FA baada ya kufanya tukio ambalo liko nje ya wachezaji kwani ameingia sehemu ambayo wachezaji hawaruhusiwi kupita na kwenda kuleta fujo.

Baada ya kocha wake Mourinho kuulizwa kuhusu tukio hilo alisema kuwa “Sidhani kama tukio hilo lilikuwa ndani ya mchezo maana Mchezo ulikuwa mzuri sana lakini siwezi kukimbia swali. “Nadhani Eric Dier alichokifanya kipo tofauti kabila na tabia za Maprofesheno, hatuwezi kufanya lakini mtu akikutukania familia yako huwa kuna hali fulani ya utofauti hutokea haswa kaka yako.”

https://www.instagram.com/p/B9Wb7L5BQID/

By Ally Juma.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents