Michezo
Mchezaji wa zamani wa Aston Villa, Dalian Atkinson auawa na polisi
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Aston Villa, Dalian Atkinson ameuawa baada ya polisi kumshambulia na bunduki ya shoti ya umeme, Taser.
Kwa mujibu wa Mail Online, maafisa waliitwa kutoka kituo cha polisi cha West Mercia kwenye nyumba ya Telford, Uingereza usiku kwa wito wa kuangalia usalama wa mtu.
Walipofika, Taser ilitumika kwa Atkinson. Mchezaji huyo alipewa matibabu lakini alitangaza kufariki baadaye.
Polisi wa West Mercia wamesema hawawezi kusema chochote kutokana na suala hilo kupelekewa kwenye tume huru ya malalamiko ya polisi.
Polisi akiwa na Taser