Mchezo wa Napoli na Lazio waahirishwa kutoka na ubaguzi wa rangi
Ligi ya Serie A iliendelea jana Feb 3 kati timu za Lazio na Napoli mchezo huo ilibidi uahirishwe baada ya kutokea vitendo vya ubaguzi wa rangi vilivyokuwa vikifanywa na mashabiki wa Lazio kwa beki wa kati wa Napoli half Kalidou Koulibaly.
Beki wa kati wa Napoli half Kalidou Koulibaly ambaye alikuwa akifanyiwa vitendo vya kibaguzi.
Ripoti kutoka kwenye mchezo huo zinasema kwamba, palikuwa na kelele za kumfananisha beki huyo na nyani zilikuwa zikipigwa na mashabiki wa Lazio kutoka kwenye majukwaa ikabidi mwamuzi kuamua kuumaliza mchezo huo uliokuwa umefikia dakika ya 68 huku Napoli ikiwa mbele kwa bao 2-0 ambayo yalifungwa na Gonzalo Higuan na Jose Callejon.
Lazio wakakumbana na adhabu kubwa ya fine kutokana na tabia iliyofanywa na mashabiki wake.
Boss wa Napoli Maurizio Sarri amempongeza mwamuzi Massimiliano Irrati wa mchezo huo kwa kuusimamisha mchezo kisha akasema alikuwa anajisikia vibaya kusikia kelele za kibaguzi kwenda kwa Koulibaly.