Habari

Mchungaji wa Muna amtaka arudiane na mumewe na kuwaonya watu wa mitandaoni ‘kaeni mbali Mungu anamakusudi yake’ (+video)

Mchungaji wa Muna Love na marehemu mtoto wake Patrick amewasihi warudiane na mumewe wa ndoa kwani msiba wa mtoto wao ni fundisho tosha.

Mchungaji huyo pia amewapiga mkwara watu wa mitandaoni na vyombo vya habari vinavyorusha habari za kupotosha kuhusu mauti ya Patrick na kuwambia kuwa mtoto huyo alikuwa ni mtoto wa Mungu na  hakuna lolote baya kutoka kwa walimwengu bali amefariki kwa mipango yake.

Hayo yote yamesemwa leo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam ambako shughuli za kuuaga mwili wa mtoto Patrick zimefanyika leo Julai 7, 2018.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents