Michezo

Mechi yetu na Singida United siyo nyepesi -Manara

Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa mechi yao ijayo ya ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Singida United haitokuwa nyepesi kwakuwa timu hiyo inakikosi kizuri.

Manara ameyasema hayo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram huku akiwataka wapenzi wa klabu ya Simba kuiombea timu hiyo iweze kuibuka na alama tatu muhimu.

Kuhusu mechi ijayo…. baada ya kupona majeraha yake Emmanuel Okwi aanza mazoezi leo mjini Morogoro….Mechi ijayo dhidi ya Singida sio nyepesi,tunawaheshimu na tunajua wana team nzuri lakini Inshaallah tutapata matokeo mazuri..Dua na Sala zenu wanasimba wote

Kuelekea katika mchezo huo unao tarajiwa kupigwa siku ya Alhamisi ya Januari 18, mshambuliaji wao hatari wa Uganda tayari hapo jana amejiunga na kikosi na kuanza mazoezi baada ya kusumbuliwa na majeraha kwa muda.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents