Habari
Mel B (Spice Girls) kulia Christmas Rwanda nyumbani (ikulu) kwa Rais Kagame
Mwaka huu muimbaji wa zamani wa kundi la Spice Girls la Uingereza, Melanie Janine Brown aka Mel B atakula sikukuu ya Christmas nchini Rwanda. Atafikia nyumbani (ikulu) kwa Rais Paul Kagame.
“Christmas ipo tofauti kila mwaka,” aliliambia gazeti la Daily Mirror wiki hii. “Mwaka jana tulikuwa Australia na ilikuwa nzuri, lakini mwaka huu tumeamua kwenda Rwanda na tutakaa kwa rais Paul Kagame.”
Mwaliko huo Mel B aliupata kupitia watoto wawili wa Kagame wanaoishi New York, Marekani.