Michezo

Memphis Depay azua gumzo katika tuzo ya mchezaji bora Ufaransa

Mshambuliaji wa klabu ya Lyon, Memphis Depay, amepokea tuzo yake ya bao bora la mwaka. Wakati akienda kupokea tuzo hiyo ya heshima, ameonekana kuvalia Jacket lake mithili ya Msanii nguli wa Pop Duniani, Michael Jackson.

Nyota huyo wa timu ya taifa ya Uholanzi amenyakuwa tuzo hiyo baada ya kufunga bao akiwa umbali wa nusu ya Uwanja.

Depay mwenye umri wa miaka 23 amekuwa na mafanikio toka alipoondoka katika klabu ya Manchester United na kujiunga na klabu ya Lyon ya Ufaransa. Muonekano wake katika tuzo hizo umewaduwaza walio wengi na kuwavutia Ukimbini hapo kwa namna alivyovalia ikiwa ni jambo ambalo halikutarajiwa na wengi.

Nyota wa zamani wa Uholanzi Frank de beor aliwahi kumuonya Depay kwa kumtaka aweke akili yake zaidi uwanjani kabla ya kujiingiza katika mambo mengine ya nje ya uwanja.

Baada ya kufunga mabao 5 katika michezo 15 aliyoingia uwanjani, ni wazi sasa Depay anahisi ni muda wake muafaka way yeye kurudi katika ulimwengu wake wa mitindo anaoonekana kukosa kwa muda mrefu sasa.

BY HAMZA FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents