Michezo
Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho ashtakiwa na FA
Kocha wa Chelsea asiyeishiwa vituko, Jose Mourinho ameshtakiwa na chama cha soka cha England, FA kufuatia madai yake kuwa kuna ‘kampeni’ ya waamuzi dhidi ya timu yake.
Mourinho alitoa matamshi hayo baada ya Chelsea kunyimwa penati dhidi ya Southampton Disemba 28 katika mchezo uliomalizika kwa sare ya 1-1.
Mwamuzi Anthony Taylor alimuonesha kadi ya manjano Cesc Fabegas baada ya kuanguka ndani ya boksi wakati akikabiliwa na Matt Targett.
Mourinho anatakiwa hadi Januari 13 kujibu mashtaka hayo.