Burudani
Mense atoka na Mix tap ya one after one
Bada ya msuguano wa hapa na pale kati ya Mense na Mexicana Lacavera hatmaye kila mmoja kula hamsini zake, Mense Selekta ameamua kuja na Mix Tap yenye vigongo 25.
Mense ambaye ni mwimbaji na Producer wa De fatility International Music, amesema wasanii kibao kwa pamoja watakuwa ndani ya Mix tape hiyo inayokwenda kwa jina la ONE AFTER ONE.
Alisema miongoni mwa wasanii ambao, watatupia , mistari yao humo ni Tash alikuwa ni mshindi wa kwanza kwenye mashindano ya freestyle katika mkoa wa Arusha, Veej, O-key, Juru, Fidodido na Emmar.