Messi ammwagia sifa Ronaldo kujiunga na Juventus asema haya kuhusu Madrid
Messi ammwagia sifa Ronaldo kujiunga na Juventus asema haya kuhusu Madrid
Mshindi wa tuzo ya Ballon d’or mara tano pia mchezaji wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusiana na uamuzi wa Mreno Cristiano Ronaldo kutimuka Real Madrid na kujiunga na mabibi kizee wa Turin Juventus.
Messi amefunguka hayo wakati akiongea na kituo cha Radio cha Catalunya na kusema:-
“Real Madrid ni mojawapo ya timu bora sana duniani na wana kikosi kikubwa, lakini inaonekana kuwa wana ukosefu wa kujiamini bila Ronaldo kwani Ronaldo kuondoka kumewafanya kuwa duni na kuifanya Juventus kuwa mojawapo ya timu zinzotegemewa kushinda Ligi ya Mabingwa UEFA ”
Messi aliongeza juu ya kuondoka kwa Ronaldo kutoka Santiago Bernabeu: “Nilishangaa sana na kunishtua alipoondoka Bernabu, Sikufikiria kuondoka Madrid na kujiunga na Juventus kwani Kulikuwa na timu nyingi zilizomtaka hicho ndio kushangaa kwangu, lakini sio vibaya maana ameenda kwenye timu nzuri sana. ”
Lakini pia akiongelea kuhusiana na mchezo wao wa El Clasco Messi alisema:- Anaamini Barcelona anaweza kuchukua faida ya kufanya vizuri dhidi ya wapinzani wao katika mchezo wa El Clasico kwani wapinzani wao hawana nguvu kama waliyokuwa nao, lakini pia anajua kuwa jitihada zote Ubingwa wa Ulaya unaweza ukatimukia huko Turin kwani kuna nguvu ya ziada imefanyika.
FC Barcelona wanaongoza ligi kuu nchini Uhispania kwa kuwa na alama 9 sawa na Real Madrid lakini wakiwa na tofauti ya magoli ya kufunga Barcelona akifunga goli 12 na kufungwa goli 2 huku Madrid wakifunga goli 10 na kufungwa goli 2.
By Ally Juma
Lionel Messi amesema kuwa kuondoka kwa Ronaldo Real Madrid kumeifanya Club hiyo ipungue makali yake na kuifanya Club ya Juventus kuwa katika nafasi nzuri ya kuchukua kikombe cha UEFA Champions League msimu huu.
Hana lolote huyo messi, madrid hiko vizur rangu alipoondoka Cristianoo Ronaldo kwa tunaofuatilia mpira
Msabaha Kassa nani kahongwa